In Creative Corner, poetry

Vumbi la mahangaiko, na kelele za uchovu
Hunitia hamaniko, kuzidi ukakamavu
Leo niko kesho siko, mambo yataka utuvu
Siku huanza, kwa makelele na vishindo

Dunia ni mzunguko, haitaki udumavu
Tete wademao koko, huchomwa wawe majivu
Imara kama mikoko, huwalinda zao mbavu
Siku huanza, kwa harubu ya uwindo

Zitakuenea mboko, zivunje chako kidevu
Wakukimbie wenzako, walo na choyo na wivu
Dunia ya masumbuko, hutuvuta kama wavu
Siku huanza, kwa midomo ya uvundo

Afrika ndipo tulipo, nisikize kwa utuvu
Kwa kutofuata miko, kutwa tunashika shavu
Ama hili sikitiko, hututia udumavu
Siku huanza, kwa riziki ya mgando

Silaha za milipuko, zinoua usikivu
Zinoharibu masoko, ya kunde na ndizi mbivu
Zimetupwaya mbeleko, nyoyo zimejaa kovu
Siku huanza, kwa tabu na nyingi nyodo

Karafuu na Choroko, tele zimejaa kuvu
Wa kuziuza hawako, wamebakia mafuvu
Vita ni letu anguko, kisha twaitwa wavivu
Siku huanza, taratibu wake mwendo

Kaditama sikitiko, ndimi askari shupavu
Sipajui niendako, naushinda ulegevu
Afrika yangu na yako, tuwashinde waonevu
Siku huanza, kwa tamaa zilo kando.

 

This poem was published in the 7th Issue of PoeticAfrica magazine.
Please click here to download.

Read – Aumwapo – Mfaume Hamisi (Tanzania)

Read – Time is Now – Nakut Janet (Kenya)


This Magazine is published by a team of professionals and downloadable for free. If you would like to support our work, please buy us coffee –  https://www.buymeacoffee.com/wsamagazine

 

 

Recommended Posts

Leave a Comment

Contact Us

We're not around right now. But you can send us an email and we'll get back to you, asap.

Not readable? Change text. captcha txt

Siku Huanza – Hafidhi Kido-Bakungwi (Tanzania)

Time to read: 1 min
0
friendshipFriend